Pages

Monday, 17 November 2014

               TUJIKUMBUSHEEE KIDOGO       

                     GOLOSO LA SOKA

                  NA YOSSIMA SITTA,  
                  0769-183981

WAJUMBE TFF WAMETAKA MABADILIKO
-Kila ukisikia kuna uchaguzi puresha na homa huwa zinapanda kwa wangombea na wapenzi wake kukiwa na wagombea wote wanaokubalika kwenye jamii. Huwa tunashudia chaguzi nyingi za siasa za CCM na CHADEMA, wakipigana vikumbo kumpata muwakilishi wake. Wajumbe wa TFF na GOLOSO walifanya kweli kuchagua viongozi wake kwani wamechagua mabadiliko. Wajumbe wa kolamu hii ya goloso walichagua viongozi wao wa Goloso(g9) katika nafasi za mwenyekiti, katibu na mhasibu. Ama kweli wajumbe wa goloso (wazee wa ting) walichagua mabadiliko Attu Gervas(Cahil) aliibuka kidedea kuwa mwenyekiti kwa kuwashida wenzake Kway Yudathadei(Vidic), Erick Gwakisa (Evra) huku nafasi ya katibu ikienda kwa kiungo matata Rajabu Juma(Wilshere) na kuwashida Danny Justine (Chicharito) na Lukuba Endrew (Januzaj). Mshambuliaji ambaye mkataba wake unaelekea ukingoni Lewandowski (Masala Yohana) aliibuka kuwa mhasibu na msemaji wa Goloso na kuwaacha kwa mbali sana Ngully Alex (Mata) na Molla Jerome (Cech).
-Narudi kwa wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF waliomchagua mwenyekiti mpya Jamal Malinzi kuwa rais mpya wa TFF kwa kura 73 dhidi ya mpinzani wake pekee Athuman Jumanne Nyamlani aliyepata kula 52. Huku nafasi ya makamu wa Rais ikienda kwa Wallace Peter Karia aliyepata kura 67 na kuwashida Ramadhani Omari Nassibu kura 52 huku Iman Madega akipata kura 6. Wajumbe walichoshwa na mizengwe ya TFF na kuamua kuchagua mabadiliko. Namkumbuka ndugu yangu Michael Wambura huwa anawekewa pingaminzi kila chaguzi ambaye uchaguzi wa kwanza ulisitishwa baada ya yeye na Rais mpya wa TFF kuenguliwa kwenye uchanguzi. Naamin angekuwepo kwenye uchaguzi huu angeibuka kidedea naye maana wajumbe wa mkutao mkuu wa TFF walichoshwa na mizengwe iliyokuwa inaendelea ndani na nje ya TFF na kuamua kuchangua mabadiliko.
-Jamal malinzi nilimnukuu akisema, “nawashukuru wajumbe wa mkutano mkuu wa TFF kwa kunikubali na kunichagua mimi jamal malinzi niwe rais wa TFF, ama kweli dunia imekuwa kijiji kwani ndani ya masaa 72 baada ya kuzindua ilani ya uchaguzi  nimepokea salamu, maoni na mapendekezo toka ndani na nje ya Tanzania ikiwa pamoja ni Burundi, Ivory Coast, Denmark na NewZealand hatimaye tumechagua mabadiliko” mwisho wa kunukuu.


-Nilisoma vizuri sera na ilani za viongozi wote wawili Nyamlani na Malinzi sikuona kosa kwa wajumbe wa mkutano wa TFF kuchagua mabadiliko. Imebaki kazi ya Rais mpya kutekeleza ilani yake alianza kwa kutoa msamaha kwa watu wote waliokuwa wamefungiwa kuanzia ngazi ya wilaya , mkoa na TFF lakini msamaha huo hauwahusu wale waliofungiwa kwa makosa ya rushwa na kupanga matokeo , pia msamaha huo hauhusu adhabu zilizotolewa katika ngazi ya klabu. Ni kazi nzuri Rais wa mabadiliko.
-Wajumbe wakaenda mbali sana wakiwa wanataka kuchagua mabadiliko. Kanda ya soka la Tanzania wakamchangua mpiganaji Kidao Wilfred Mzigama kuwakilisha kanda ya 13 Dar es Salaam. Kidao alihangaika sana kwenye kamati kuvuka ila dakika za mwisho mwisho akavuka na jamaa yake Shaffih Dauda akatupwa nje. Mwisho wa siku wajumbe wakachagua mabadiliko.
-Rais aliyemaliza muda wake leodegar tenga tangu 2004 mpaka 2013 ameacha mazuri na mabaya, imebaki kazi ya Jamal malinzi kuyaacha ya akina Agape Fue na kuendeleza mazuri yaliyoachwa na tenga .Pia kuyaacha mabaya yote ya akina Tenga, Nyamulani na timu yake.
                       mwandishi wa makala hii ni yocma sitta mhariri wa goloso 
makala hii ilikuwa ya wakati wa uchaguzi wa TFF

0 comments:

Post a Comment