Pages

Thursday, 6 March 2014

ARSENAL FC YA LEO NA ILE TUNAYOITARAJIA


                         GOLOSO LA SOKA 
Na  Kway Yudathadei

Arsenal ni kati ya klabu kubwa,maarufu,yenye uwezo kifedha  na zaidi yenye mashabiki lukuki katika kona mbali za sayari hii ya Dunia nisijue zaidi hata nje ya mipaka ya dunia hii.Ni mengi yanaweza kuzungumziwa kuhusu klabu hii lakini nitapenda kuyaweka hadharani katika dawati hili la soka machache  tu ninayohisi yataweza kuwagusa wadau .
Klabu hii ni ya mpira wa miguu(soka) yenye maskani yake katika  eneo liitwalo Holloway huko kusini mwa Jiji la London na ilianzishwa mnamo mwaka 1886 japokua mafanikio yake yalianza kuonekana zaidi katika miaka ya 1930.
Katika kuitazama Arsenal ya  kuanzia mwaka 2000 hadi mwaka 2014 yako machache ya kusemea.Klabu hii imeweza kupata mataji mawili tu ya ligi kuu ya nchini Uingereza na mataji hayo yalipatikana katika misimu ya 2001/2002 na 2003/2004.Hizi ni enzi ambazo Arsenal FC waliweza kuijulisha dunia ni kwa jinsi gani wanaweza kulitandaza soka sio tu kuishia kupiga pasi zenye macho ila hata kupachika mabao na kuzuia wapinzani wao kupitia mabeki mahiri kabisa waliokuwa nao enzi hizo.
Arsene Wenger ni kocha aliye kabidhiwa majukumu ya kuinoa timu hio katika mwaka 1996 na alidhihirisha ubora wake  kwani ukiachana na kuchukua kombe la ligi kuu miaka miwili baada ya yeye kuanza kuinoa timu hio na hata kufanya usajili wenye manufaa kwa kuwanunua wachezaji makini kama Patrick Vieira,Emmanuel Petit,Marc Overmars,Nicolas Anelka na  wengineo wengi,mwaka 2000 aliiwezesha timu hio kufika katika hatua ya Fainali ya kombe la mabingwabarani Ulaya,aliendeleza ubabe kwa kuchukua kombe la ligi kuu nchini Uingereza katika mwaka 2002 na 2004 kabla ya kufikia hatua ya fainali kwa mara nyingine ya kombe la UEFA hapo 2006 dhidi ya Barcelona FC katika jiji la Paris nchini Ufaransa pale Stade de France akiwa na wachezaji mahiri kabisa kama Thiery Henry,Robert Pires,Gilberto Silva,Fredrik Ljungberg,Ashley Cole,Jens Lehman na wengnineo,enzi izo Van Persie,Gael Clichy,Dennis Bergkamp,Jose Antonio Reyes,Plilippe Senderos,Flamini  wakisuburi benchi .
Katika kipindi hiki chote Arsenal ilikua ni timu yenye wachezaji mahiri na wenye kuimiri vishindo,kashkash na mikikimikiki ya ligi kuu na hata ile ya ligi bora kabisa duniani,ligi ya mabingwa katika nchi za Ulaya.
Miaka michache baadaya klabu hii hii chini ya kocha wake  huyuhuyu,dunia imeshuhudia madiliko hasi kwani klabu hii imegeuka kuwa mithiri ya kiwanda cha kuzalisha vipaji na kisha kuwauza katika vilabu vikubwa vyenye kutoa vitita vya pesa na zaidi,vilabu vyenye kiu na mataji.Hii imepelekea kumuangalia Wenger katika jicho jingine kabisa,hili ni jicho la ubahiri au kiutaalamu akiitwa mchumi na walio wengi,sababu za watu kuamua kumuita hivyo ni kutokana na yanayoendelea klabuni hapo,kuwauza wachezaji makini na wenye jeuri ya kuiletea klabu vikombe na kuacha kusajili wachezaji wenye hadhi ya kushindana na timu kubwa akisingizia katika miaka michache iliopita kuwa anafanya kukuza vipaji vitakavyoweza kuitetea klabu hio katika miaka ya usoni,lakini tunalo lishuhudia ni wachezaji kukua na wale walio bora zaidi kuuzwa katika vilabu vikubwa.Hii inatoa picha mbili,kiuchumi ni kweli klabu inanufaika kwa kupata faida kubwa kwani mishahara anayowalipa wachezaji walio wengi ni midogo na bado akiwauza wachezaji anawauza kwa pesa nyingi lakini katika upande wa pili wa shilingi anawaumiza mashabiki wa klabu hii kwani wanaishia kushuhudia timu nyingine zilizo makini zikibeba vikombe.
Soka la leo linahitaji Pesa kama kitu cha kwanza.Arsenal FC ni klabu yenye pesa lakini matumizi yake hayaonekani zaidi machoni pa wadau kama klabu nyingine kubwa zifanyavyo katika soka la leo.Katika miaka ya hivi karibuni tumeshuhudia jeuri ya pesa katika kuleta mapinduzi,Manchester City FC wameweza kuleta mapinduzi katika ligi kuu nchini Uingereza na hata katika zile klabu nne bora, ‘’big four’’ kukitokea upinzani wa aina  yake,bado tumeweza kushuhudia huko nchini Ufaransa PSG pamoja na Monaco zinavyofanya mapinduzi,yote hii ikiwa ni jeuri ya pesa.
Machache ya kumalizia kuhusu klabu hii na hasa kupitia meneja wake,ni kutambua alama za nyakati  na kuwatendea haki mashabiki wake.Pesa ndio silaa pekee katika kupata wachezaji makini na mwisho wa siku kubeba vikombe.

mwandishi wa makala hii na msanifu wa goloso kwa habari za kimataifa

0 comments:

Post a Comment