Pages

Sunday, 9 March 2014

NANI KAMA DAVID MOYES….????


             GOLOSO LA SOKA

          Na yudathadei kway
                   0768-154424
Nianze kwa kuwasabahi, kila mdau kwa nafasi yake.Ni kwa mara nyingine tunakutana hapa kijiweni katika dawati hili la michezo na burudani tukijaribu kuumiza bongo zetu.Basi leo ninakuja na mada ya moto kati ya mada za moto  nje ya mipaka ya nchi yetu hususani katika Bara la Ulaya,bara linaloonekana kua na mvuto zaidi katika tasnia hii ya soka na zaidi tukijikita katika viunga vya jiji la Manchester katika klabu kongwe ya Manchester United FC.

Klabu hii ilianzishwa hapo mwaka 1878 na kuitwa Newton Heath LYR Football Club na mnamo mwaka 1902 jina likabadilishwa na kuwa Manchester United.Klabu hii imekua na mafanikio makubwa chini ya makocha mbalimbali wakiwa wameharibu rekodi zilizowekwa na makocha wengine lakini pia wakiweka na wengine kuvunja rekodi katika klabu hii kongwe.

Leo hii ni katika kumuangazia kocha wa sasa David Moyes aliye rithi mkoba ya babu Sir Alex Ferguson.Moyes amekua na wakati mgumu sana kiujumla katika klabu hii ya Greater Manchester na hii imechochewa na sababu mbalimbali kulingana na mitazamo na maono ya wadau tofautitofauti.Katika kupunguza ukosefu wa vithibitisho,basi tujaribu kuzitazama rekodi mbalimbali alizoweka kwa kuharibu za zamani lakini pia tuziangalie zilezilizovunjwa na meneja huyu

Rekodi ya kwanza kuwekwa na kocha huyu ni ile ya kuwa kocha wa kwanza kabisa kuanza majukumu yake na kubeba kikombe,Ilikua mnamo tarehe 11 mwezi wa nane ambapo magoli mawili ya mpachika magoli mahiri Robin Van Persie alipowatungua Wigan magoli mawili bila na kuiwezesha klabu yake kutwaa  ngao ya hisani.

Rekodi nyingne ni ile iliyowekwa na klabu hii chini ya kocha wake huyu ya kushinda mechi yake ya kwanza ya ligi kuu nchini uingereza tokea mwaka 1977 timu hii ilipokuwa chini ya kocha Dave Sexton. Rekodi hii iliwekwa katika dimba la Liberty Stadium likitazamwa na mashabiki wapatao 20,733 kwa Manchester United kuichabanga Swansea magoli manne kwa moja.

Lakini pia kocha huyu ameiwezesha klabu hii kupata ushindi mnono ugenini katika makombe yanayo shirikisha vilabu vya Ulaya tokea hapo mwaka 1957 ambapo kocha Busly Babes alipoiadhibu Ireland’s Shamrock Rovers kwa magoli sita bila.Moyes amekuja kukumbushia hayo kwa kuiongoza timu yake kuilabua klabu ya nchini ujerumani,Bayer Leverkusen kwa magoli matano bila hapo tarehe 27 ya mwezi wa kumi na moja

Kocha huyu pia ameweza kuvunja rekodi zilizowekwa na makochawengine katika klabu hii kwa kumsainisha mkataba mnono katika klabu hio na hata katika klabu nyingine zote katika ligi kuu ya Uingereza mchezaji wake Wayne Rooney.Mchezaji huyo raia wa uingereza amesaini mkataba wa kumfunga klabuni hapo kwa miaka mitano na nusu akiwa analipwa paundi 300000 kwa wiki na katika kipindi chote cha mkataba kusadikika kupata paundi milioni 85.

Rekodi nyingine aliyowekwa ni ile ya kumsajili kiungo mshambuliaji Juan Mata kutoka katika klabu ya Chelsea FC kwa kitita cha paundi milioni 37.1 na kuvunja rekodi ya uhamisho klabuni hapo mnamo mwaka 2008 kwa Sir Alex kumsajili kutoka Totenham mchezaji Dimitar Berbatov kwa kitita cha paundi milioni 30.75.Ikiunganishwa na uhamisho wa kiungo mkabaji Marouane Fellaini kutoka Everton katika majira ya joto ulioighaimu klabu ya Man U paundi milioni 27.5,David Moyes anaweka rekodi nyingine kwa kutumia kiasi kikubwa kabisa cha pesa katika msimu mmoja kipatacho paundi milioni 64.6.

Kocha huyu pia ameweza kuweka rekodi mbovu klabuni hapo katika msimu wake wa kwanza katika kuinoa klabu hii na kua katika ya vigezo hasi kwa wadau wa soka mpaka kuanza kuutilia mashaka ufanisi wake wa kazi kulinganisha na makocha wengine,rekodi hizi ziko hapa chini katika mapana yake

Mpaka sasaivi klabu hii kongwe imefungwa mechi zipatazo nane katika ligi kuu na bado ikiwa na kibarua kikubwa katika mechi za usoni.Tukirejea karika historia ya klabu hii inaonekana katika misimu miwili,ya 2001-2002 na 2003-2004 klabu hii ilipoteza mechi tisa kila msimu lakini bado ilimaliza ikiwa nafasi ya tatu katika kila msimu.Tusubiri mpaka mwisho wa msimuilituone  itakuaje.

Rekodi nyingine mbaya kwa kocha huyu ni ile ya Manchester city FC kuiadhibu man U magoli manne kwa moja katika dimba la Etihad.Kwa mara ya mwisho ilitokea katika dimba hilohilo mnamo mwaka wa 1989 ambapo Man U waliadhibiwa vikali kwa magoli matano kwa moja.

Kuthibitisha ni jinsi gani mpaka timu ndogo kimafanikio zinavojizolea sifa kutoka kwa mashabiki wao na hata kuwapa mashabiki wa timu pinzani na man U kupata mwanya wa kuiogelea vibaya timu hii,Klabu ya Stoke City,the potters imefanikiwa kuichachatya man U katika msimu huu,mara yao ya mwisho ikiwa ni mwaka 1984.

Lakini pia Newcastle United kupitia mshambuliaji wake Yohan Cabaye,imeweza kukata kiu yake ya miaka 41 bila kuifunga Manchester united katika dimba la Old Trafford.Katika mechi zipatazo 32 man U wamekua wakiibuka washindi lakini Cabaye aliweza kuharibu rekodi hii chini ya kocha David Moyes.

Katika michuano ya vilabu barani ulaya,David Moyes amezidi kujiharibia sifa klabuni hapo kwa kipigo cha mbili bila kutoka kwa klabu ya Olympiakos katika hatua ya 16 bora na hivyo  kuwa klabu ya kwanza ya ugiriki kuifunga Man U katika hatua hii.

Katika kuhitimisha,sitaki kutoa tamko lolote kumhusu David Moyes kwani nahisi bado ni mapema sana kulingana na uhalisia wa klabu ya Man U kwa makocha wake kihistoria.Lakusema hapa ni moja tu kulingana na uhalisia wa soka,iwe timu ya klabu au timu ya taifa,’’Soka ni sawa na mashua baharini,mawimbi yakitanda mashua hupata wakati mgumu katika safari yake  mithiri ya tumbo kuvurugika na mawimbi yakitulia hali hua shwari’’.Tukutane kijiweni wakati mwingine wadau,Hili ndilo dawati la soka bhana.

mwadishi wa makala hii ni msanifu wa habari za kimataifa wa goloso

0 comments:

Post a Comment