Pages

Thursday, 26 December 2013

16 BORA YENYE MASHIKO UEFA

          
 GOLOSO LA SPORT
NA YUDATHADEI KWAY
Ligi ya mabingwa ulaya ndio inayosadikika kuwa ligi bora kabisa duniani inayotoa kila aina ya ladha ya mpira huu gumzo duniani,mpira wa miguu.Ndio ligi inayowakutanisha ma supastaa wa aina hii ya mchezo.
Katika msimu huu wa hii ligi mengi yameshuhudiwa na wadau wa tasnia hii ya mchezo katika hatua ya mwanzo kabisa ya michuano hii ambapo baadhi ya vilabu vikubwa kama Napoli, Olympic  Marseille, Juventus, FC Porto, Benifica, Ajax vikisogezwa kando na hatua za juu za michuano hii lakini pia vilabu vingine vikiingia katika hatua inayofuata.Draw imefanyika na hatimaye kila moja wapo ya kilabu imeshafahamu itavaana na nani.
Hakika mengi yamefikirika, mengi yamezungumzwa nabado yanazungumzwa juu ya matokeo ya  hii draw.Sitataka kugusia juu ya kila klabu na kitakaekutana naye bali lengo langu ni kujaribu kugusia vilabu  vya EPL vinavyoteka na kukonga nyoyo za watanzania walio wengi

Nikianza na Arsenal FC, washika mtutu wa Jiji la London ktika viunga vya Highbury; hakika hii ni klabu iliozoea hii ligi kupitia kocha wake Arsene Wenger. Katika msimu huu wa EPL imeweza kuonyesha ni jinsi gani ilivyo makinika na hata kuongoza ligi kuu yaUingereza mpaka hivi leo mengi yameongelewa kuhusu chachu walio nayo hivi sasa na baadhi wamethubutu kutoa maoni yao kama vile,ujio wa kijana machachari kabisa mwenye kujua kulitumia guu lake la kushoto vilivyo katika kupiga chenga na kupenyeza ngome za timu mbalimbali lakini zaidi katika kupiga pasi za mwisho,hapa ninamzungumzia mjerumani mwenye asili ya kituruki Mesut Ozil alie tokea Real Madrid lakini wengine  wanatoa maoni yao na kudai ni kwa sababu ya kujiamini kwa Kocha wake mzee Wenger hasahasa baada ya Babu Sir Alex Ferguson kustaafu na Wenger kubakia kama kocha mkongwe aliedumu na klabu yake kwa mda mrefu inayo ambatana na kuchipukia kwa safu ya kiungo yenye morali ya kutosha ya vijana Carzola,Wilshere, Ramsey wakiongozwa na kamanda wao Mesut Ozil. Klabu hii imeweza kupenyeza hata katika kundi lililosemekana ni la kifo katika hatua ya kwanza ya ligi ya mabingwa ulaya lililokua na timu za Dortmund, Napoli, Marseille na Arsenal. Katika hatua hii ya 16 bora wamekutanishwa na miamba ya soko na bingwa watetezi Bayern Muchen, Vijana wanaopiga soka la kiufundi, soka lenye taaluma kiufundi katika Nyanja ya pasi, kasi na nguvu.klabu yenye wachezaji machachari wenye uchu na ushindi katika kila game wanayocheza, akina Frank Ribery, Robben, Muller, Gotze, Larm na wengineo wengi. Mengi yanaongelewa lakini yote katika yote ni kusubiria kitakachojiri.


Tukiwageukia Vijana wengine wa Jiji la London, the blues  walio chini ya kocha maarufu, kocha mtabe, kocha mwenye kuthubutu kujaribu, kocha jeuri Jose Mourinho. Ni kati ya timu zinazoogopeka katika michuano hii kwani ina vijana wenye vipaji na wenye hamasa kubwa ya mataji inayochochewa na kocha wao Mourho. Imefanikiwa pia kufikia hatua ya kumi na sita bora ambapo imepangwa na Klabu yenye uwezo pia ya Galatasary kutokea Uturuki. Kukutana kwa timu hizi kunazua hisia kali za kutamani kushuhudia tifu lake kwasababu chache kama, Didier Drogba kijana alieifanyia makubwa klabu ya Chelsea akiwa chini ya Mou na hata baada ya Mou kuondoka bado akaisaidia klabu yake kubeba ubingwa wa UEFA mwaka 2012 na kuinyang’anya bayern muchen tonge mdomoni katika uwanja wake wa nyumbani, lakini pia ni kukutana wakiwa na timu mbili tofauti kocha Mou na Kijana fundi wa kiholanzi Sneijder waliokua wote katika klabu ya International Milan na wakifanikiwa kuchukua kombe la mabingwa la Ulaya mwaka 2009 bila kusahau hamu ya kuona maajabu ya kocha Mancini akiwa na kikosi cha miamba hio ya Uturuki.Tungojee kwa hamu maajabu ya mitanange hio ninayoiita shupavu kwani timu hizi zote zina aina flani inayofanana kimchezo kwa kutumia nguvu.

Katika kuwaangalia Man City FC kutokea katika mitaa ya jiji la Manchester, Hii ni klabu ilio na wachezaji mafundi na wenye kila aina ya mbinu ya kuikabili timu yoyote ile chini ya kocha wake Pellagrin. Katika hatua ya 16 bora wamepata kupangwa na timu machachari kabisa katika kupiga pasi za kifundi na kumiliki mpira watakavyo wao, hawa ni vijana wa Catalunya Barcelona FC. miamba hii miwili inavuta hisia za wakereketwa wa kandanda kwani wote wawili wako katika hari mahiri kabisa ya kuchukua mataji,wakiongozwa na makocha wenye hekima ya kisoka na wenye kila sababu ya kushinda kila mechi inayokua mbele yao kwa maana ya kua na zana zenye makali ya kutosha lakini chachu nyingine inaletwa na uwepo wa kijana mwenye tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika Yaya Toure alietokea Barcelona na kutua Man City na kuonyesha kiwango bora kabisa na hata kusababisha maswali mengi kwa wadau wa soka, Je ni kweli Barca walimuuza kwa kua alikua ameshuka kiwango? Je ni kweli Sergio anakiwango cha kuweza kuchochea kuuzwa kwa Yaya? Yote haya yanaweza jibiwa vyema kabisa na matches watakazokutana. Hatatumwa mtoto dukani hapo .

Mabingwa watetezi wa EPL Manchester United nao wako katika hatua hii ya 16 bora. Ni klabu ambayo iko katika hatua au kipindi ambacho waingereza wanakiita ‘’transitional period’’ wakimaanisha kipindi cha mpito. Hii inasababishwa na kusadikika kwa kupungua kwa makali ya klabu hio baada ya kustaafu kwa kocha wake Sir Alex na mikoba yake kukabidhiwa David Moyes ambae mpaka sasaivi hajaonyesha kile ambacho mashabiki wa klabu hii wamekua wakikizoea kipindi kile akiwepo babu Ferguson. Kwa sasa klabu hii inashikilia nafasi ya 8 katika EPL jambo ambalo halikua rahisi kutokea kipindi cha Sir Alex katika kipindi hiki cha Christmass.Wadau wanadai kocha huyu apewe muda kwani mafanikio kimpira sio jambo la upesi. Basi katika hatua hii ya 16 bora wamekabidhiwa vijana wa kigiriki. Olympiacos wenye uzoefu na michuano hii na wenye uwezo pia kimpira. yetu ni macho katika kutizama, akili katika kutathmini na maskio katika kusikia yatakayosemwa baada ya matches katika kulinganisha fikra na mitizamo.

Kushinda kwa timu yoyote kimpira kunategemea vitu kadhaa vikiwemo, makocha wenye hekima kisoka, machezaji wenye viwango bora kabisa wawapo katika pitch, kuridhishwa kwa makocha na wachezaji kimaslahi (uongozi bora wa vilabu) na hamasa au amshaamsha ya mashabiki.  Timu zote zinazoingia katika ligi hii ya mabingawa ulaya zinakua na vigezo vyote hivi kwamaana nyingine ni kwamba,’’zote zinakila sababu ya kushinda,hakuna timu ya kubeza’’.Tusubiri kwa hamu yatakayojiri.
0768-154424



0 comments:

Post a Comment