Pages

Thursday, 12 December 2013

LIWALO NA LIWE BRAZIL 2014



               LIWALO NA LIWE BRAZIL 2014
-Baada ya pilikapilika za kumalizia kwa mechi za mtoano hatimaye liwalo na limekuwa mataifa 32 yamefuzu kwenda kombe la dunia Brazil 2014 kwa bara la Africa wababe Ivory Coast, Cameroon, Ghana, Nigeria na Algeria, wakati bara Asia ni Australia, Japan, Iran, na Korea Kusini, huku bara lenye timu nyingi la ulaya mataifa ya Ubelgiji, Bosnia, Italia, Urusi Ugiriki, England, Ujeruman, Uswisi, Ureno, Hispania, Ufaransa, Croatia, na Uholanzi, Amerika ya kaskazini itakuwa inawakilishwa na mataifa ya Costa Rica, Honduras, Marekani na Mexico wakati bara mwenyeji kutakuwa na mataifa ya Argentina ya Messi, Colombia, Ecuador, Uruguay, Chile na mwenyeji Brazil ya Neymar
Imekua ni njozi  ya wachezaji wengi kucheza na zaidi kuonyesha makali yao katika mitanange ya kombe la dunia, kwani hata mchezaji awe  ana mafanikio makubwa kiasi gani katika klabu aliopo hua wanahisi kukamilisha ndoto yao ya mafanikio katika michuano ya kombe la dunia. Hayo yamethibitika hivi karibuni baada ya mchezaji alie katika kiwango cha juu kabisa duniani na hata kuthibitisha makali yake kwa kuchukua tuzo lukuki zikiwemo za mchezaji bora kabisa wa dunia, Leonel Messi aliekiri ya kwamba furaha yake katika soka itakamilika tu endapo ataisaidia taifa lake kuchukua kombe la dunia.
Wachezaji wanaorindima katika kabumbu la vilabu huumia sana wanapokosa nafasi ya kucheza katika michuano ya kombe la dunia hilo limeonekana kwa wachezaji wengi na mmoja wao ni Zlatan aliepatwa na kiwewe kama sio gadhabu baada timu yake ya taifa kukosa ticket ya kucheza kombe la dunia huko Brazil mwakani na kutamka ya kua, ’’michuano hio haita pata mashiko au haita noga pasipo uwepo wangu’’. Jambo ambali sitaki kuliamini sana.
Bado michuano ya kombe la dunia  hua ni nafasi tosha ya vilabu kupata kujionea vipaji kutoka katika mataifa mbali mbali,mifano iko mizuri lakini mfano uliobayana ni ule wa kinda katika enzi hizo Ronaldnho alieaminiwa na kocha wake Luiz felipe scolari kwa kumfanya mbadala wa gwiji wa soka,Romalio mbali ni vitisho na lawama za kutosha kutoka kwa wabrazil. Pia kombe la dunia pale bondeni kwa mzeee Madiba liliibua vipaji vingi vingi kama akina Suarez kwa Uruguay, Chicharito kwa Mexico, Ozil na Khedira kwa Ujerumani,
Na sasa ni wasaha mwingine tena timu zikiwa zimeshapatikana za kwenda kuwakilisha mataifa na hata mabara yao huko katika nchi maridadi kabisa kwa fukwe zenye kila aina ya nakshi nakshi na warembo maridadi kabisa bila ya kusahau kua ndio aridhi inayoamika na wengi kwa kua na vipaji vya kutosha vyenye ustadi wa hali ya juu na hata style yao aina ya samba yenye kuleta msisimko wa ajabu kwa watazamaji pindi vijana hawa wawapo katika pitch, hii ni Brazil ama kwa hakika.

Wako wachezaji wengi ambao wanafanya makubwa katika tasnia ya soka kupitia vilabu vyao, Basi michuano hio ijayo ndio itakua mzani tosha wa kutoa ukweli ni nani aliemzito zaidi katika kabumbu. Tunasubili kuona makali ya akina Falcao na Colombia yao, Hazard na Ubelgiji, Ronado na Ureno, Neymar na Brazil, Kagawa na Japani, Yaya na Ivory Coast, Ribery na Ufaransa, Messi na Argentina,  Dzeko na Bosnia, Baloteli na Italy pamoja Rooney na England na wengine wengi
Hitimisho katika haya yoooote ni jukumu letu kutayarisha akili,macho na mioyo, yote haya ni katika kutoa tathmini makini juu ya mrindimo wa michuano kabambe kabisa ya kombe la dunia.Nani atakae kua kinara katika kuthibitisha makali yake katika kulitetea taifa lake kama wengi wao wanavo pigana kufa na kupona katika vilabu vyao. Na mwisho wa siku tusubili tuone  makundi manane yatakuwaje nani nani watambana katika makundi, liwalo na liwe yaani mtoto hatumwi sokoni pale Brazil.
         by YOSSIMA SITTA (goloso 4real)

0 comments:

Post a Comment