WAKATI straika mpya wa Yanga,
Emmanuel Okwi akitua nchini tayari kuitumikia timu yake mpya, Shirikisho la
Soka la Uganda (Fufa) limesema mchezaji huyo ni halali kuichezea Yanga na ndiyo
maana walikubali kutoa hati ya uhamisho wa kimataifa (ITC).
Ofisa Mtendaji mkuu wa Fufa, Edgar
Watson ameuambia mtandao huu kwamba, anachojua kama bosi wa Fufa ni kwamba ni
kweli Okwi amesaini kuichezea Yanga na shirikisho lake limetuma ITC kwenda Tanzania
kwa Yanga ili aweze kuichezea timu hiyo.
“Kwanza nataka kuweka wazi kwamba,
Okwi alikuwa na kesi dhidi ya timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia juu ya masuala
ya mkataba, Fifa (Shirikisho la Soka la Kimataifa) lilimruhusu kucheza kwenye
klabu ambayo anaitaka kwa muda maalum.
0 comments:
Post a Comment