Pages

Friday, 20 December 2013

FIFA YAMRUHUSU OKWI KUJIUNGA NA YANGA



WAKATI straika mpya wa Yanga, Emmanuel Okwi akitua nchini tayari kuitumikia timu yake mpya, Shirikisho la Soka la Uganda (Fufa) limesema mchezaji huyo ni halali kuichezea Yanga na ndiyo maana walikubali kutoa hati ya uhamisho wa kimataifa (ITC).
Ofisa Mtendaji mkuu wa Fufa, Edgar Watson ameuambia mtandao huu kwamba, anachojua kama bosi wa Fufa ni kwamba ni kweli Okwi amesaini kuichezea Yanga na shirikisho lake limetuma ITC kwenda Tanzania kwa Yanga ili aweze kuichezea timu hiyo.
“Kwanza nataka kuweka wazi kwamba, Okwi alikuwa na kesi dhidi ya timu ya Etoile du Sahel ya Tunisia juu ya masuala ya mkataba, Fifa (Shirikisho la Soka la Kimataifa) lilimruhusu kucheza kwenye klabu ambayo anaitaka kwa muda maalum.

0 comments:

Post a Comment