Pages

Sunday, 5 January 2014

FITINA ZA OKWI NA KASEJA ZA MFUKUZA BRANDTS


                            GOLOSO LA SPORT

                      NA YOSSIMA SITTA


Nchi yetu haikosi vitimbwi kila kukicha unafiki unafiki, majungu majungu kila sehemu na kila secta hapa nchini achana na unafiki unaofanya kwenye maofisi ya serikali na yale ya umma maana bila kujuana utasubili sana, Achana na unafiki unaoendelea ndani ya chama cha Chadema na Zitto wao, Pia futa unafiki wa Diamond na mademu zake, Kila sehemu unafiki na majungu ndo habari ya mjini angalia Tff wanavyofanya kazi kifitina kuwapata viongozi wao. Usiombe kukutana na fitina za Ccm kwenye siasa za bongo lakini haya ndio maisha yetu kwa sasa mpaka sasa siasa, majungu, fitina zimeingia kwenye soka letu la Tanzania kila mtu anaamua tu anachokiamini.

Kocha mkuu wa timu ya Yanga Ernest Brandts amepewa notice ya mwezi mmoja ataamua mwenyewe kama ataendelea kuifundisha yanga ndani ya mwezi mmoja au lah, Sioni mantiki ya kufukuzwa kwa Brandts wazee wa kazi wamesema sababu ya kupewa notice ya mwezi mmoja ni kwa sababu ya kutoridhishwa na kiwango cha uchezaji wa timu yao kwenye baadhi ya mechi na mechi ya bonanza kama wanavyoita wao yaani mechi ya mtani jembe dhidi ya watani wao wa jadi Simba ambayo ilichezwa katika uwanja wa taifa na kuambulia kipigo cha mabao matatu kwa moja

Uongozi wa Yanga umefanya fitina na ili kumfukuza kazi kocha wao Ernest Brandts mengi yamesemwa na mengine yanaendelea kuibuliwa eti amefukunzwa kwa sababu timu imekosa ufanisi, Kutoridhishwa kwa uchezaji wa timu nzima, Kufungwa na Simba mechi ya mtani jembee, Kikosi kuwa na mastaa wengi na kushindwa kuifunga Simba yenye watoto wengi, ila yote yatasemwa na watu wataendelea kusema ila kilichomfukuzisha kazi kocha wa Yanga ni Emmanuel Okwi na Juma Kaseja Juma kwa nini nasema Okwi na Kaseja wamemfukuza Brendts ni kwa sababu wamesajiliwa kwa matakwa ya uongozi na si kwa mahitaji ya kocha

Huwa nazishagaa sana vilabu vyetu hasa Simba na Yanga usajili wa wachezaji huwa unafanya na viongozi na si bechi la ufundi angalia wazee wa kazi ndani ya Yanga wanavyosajili wachezaji si kwa mahitaji ya kocha bali ni kwa mahitaji ya kuwaridhisha mashabiki wao wa Yanga na kuikomoa  Simba. Ujio wa Kaseja na Okwi Yanga ni wa kishabiki zaidi na kuikomoa Simba kitu ambacho ni hatari kwa kilabu utaifunga vipi Zamarek ya Misri, Enyimba na  Tp Mazembe kwenye ligi ya mabingwa kama unasajili kishabiki zaidi, Wazee wa kazi Seaf Magari, Bin Kaleb, na Mutabara wanamwaga pesa ili kuwafurahisha mashabiki wao si wanajua mwana mkubwa Yusuf  Manji amesema hatangombea tena nafasi ya mwenyekiti wanaweza kuichukua Yanga hapo mbeleni. Wanafanya hivyo ili kuteka hisia za wapenzi na mashabibiki wa Yanga maana walishajua watanzania sisi ni wazembe wa kufikiria na kuangalia mbali leo Yanga wanashagilia uwepo wa Okwi na Kaseja na kusahau kabisa kwenda kumuuliza ahadi hata mbili tu Manji alizowaahidi wakati anaomba kura kuwa rais wa kilabu yaooo

Kila mara nilikuwa namsikiliza kocha Brandts akikataa usajili wa Kaseja maana tayari alikuwa na makipa wawili wazuri wenye hadhi ya kimataifa Ally Mustafa Bathez na Deo Munishi Dida sasa Kaseja Juma anakuja kufanya nini? kwa sababu ni chaguo la bossi wako lazima ukubali kuwa naye na ukikubali kuwa naye tena inakulazima umpange kwenye kikosi cha kwanza ili mashabiki wafurahi na wazee wa kazi waonekane wamefanya kazi ya maana la sivyo wakufute kazi ndio utamaduni wetu kwa soka letu na siasa nyingi sana. Pia kama vile timbwili lanaelekea ukingoni Brandts tena akasikia wazee wa kazi wamemalizana na Okwi, sina tatizo na kiwango cha Emmanuel Okwi na kocha yoyote atakuwa tayari kufanya kazi na okwi ila kumletea okwi matakwa ya mashabiki wao ndio alichokuwa analalama kocha maana yanga ilikuwa na viungo na winga wazuri ngassa, Msuva, Niyonzima, Chuji, Nizar, Domayo, sasa Okwi wa nini bora kidogo usajili wa kinda Shaaban dilunga.

Vilabu nyetu vimekosa mipango na uvumilivu kabisa hasa Simba na Yanga sijaona kocha anamaliza hata miaka sita kuwa kwenye bechi la ufundi. Wamekuja wengi wamefukuzwa wengi si kwa sababu ya ufundi ni kwa sababu ya unafaiki au kufungwa Simba au Yanga poleee Brandts hizi ni siasa za soka letu lakini wewe ni Professional na utabaki kuwa Professional tu.
  0769-183981

0 comments:

Post a Comment