Pages

Thursday, 23 January 2014

                       
                           GOLOSO LA SOKA

                             Na Yossima Sitta & yudathadei kway     

    SOKA KATIKA UHALISIA WAKE

Swali likiulizwa, Je ni mchezo gani maarufu zaidi duniani? Bado linabaki kuwa swali lenye utata kwa maana ya kwamba umaarufu kimchezo unaweza kuwa ;mchezo unaoangaliwa na wadau walio wengi kwa maana ya kuamasika na mchezo husika au inaweza kuwa mchezo uliochezwa kwa muda mrefu zaidi duniani au unaweza kuwa mchezo wenye kuingiza mapato zaidi duniani. Katika kulitazama hili la mchezo wenye hamasa zaidi duniani kwa kuangaliwa na kufuatiliwa na walio wengi, tafiti za kina zimefanyika kimataifa na imebainika kuwa  watu wapatao 3.3-3.5 bilioni kutoka katika mabara mbalimbali (Ulaya,Africa, Asia ,Americas ,n.k) ni wakereketwa wa mchezo wa soka, mpira wa miguu. Takwimu hizi ni kati ya jumla ya watu wanao kadiriwa kufikia billion 7.137 Dunia nzima kulingana na taarifa iliotolewa na United States Census Bureau (USCB ) hapo 12,March,2012. Tukiingia ndani zaidi  kitafiti inaonyesha  mchezo huu unakadiriwa kuchezwa na wachezaji million 250 katika nchi zipatazo 200 na kudhihirisha kuwa mchezo maarufu zaidi katika sayari hii. Michezo inayofuata kwa umashuhuri ni pamoja na Cricket wenye wakereketwa wapatao 2-3 billion. Field Hockey wenye mashabiki wanaofikia 2-2.2 billion na mchezo huu ni maarufu zaidi katika nchi za Asia, Ulaya, Australia, n.k ukifuatiwa na Tennis mchezo wenye mashabiki wapatao billion 1 zaidi katika nchi za Ulaya, Americas na Asia.
Katika kujikita kisoka zaidi kuna sababu nyingi zinazo jaribu kuthibitisha ni kitu gani kinachofanya mpaka watu kuvutiwa na mchezo huu zaidi na hata wengi wao kudiriki kukiri ya kuwa hawana sababu maalumu isipokuwa wamejikuta wakiupenda tu. Hili liko wazi hata kwa wale walio na uzoefu kama sio professionals katika uliwengu wa mapenzi mtu akimpenda mwenzi wake basi kama sio kwa sababu za tamaa tamaa tu, Huwa ni ngumu  kuwa na sababu ya moja kwa moja  iliomfanya au inayomfanya kumpenda mwenzi wake zaidi inabaki kuwa ni uhalisia usio elezeka kirahisi. Hii ndio sababu nzito zaidi kwa walio wengi katika upenzi wa mchezo huu tajwa.Tumepata kusikia matukio mengi yanayoendana na upenzi katika tasnia hii ya soka, Kama vile watu kujiua kisa timu zao kufungwa, mashabiki kuuawa kisa tu mashabiki kuwa wengi kuliko ukubwa wa uwanja. Watu kucheza kamari na hata kujivunia mengi yaliyo ya thamani na hata wengine kusadikika kuwaweka wake zao rehani kisa tu ni upenzi uliokithiri juu ya mchezo huu mashuhuri zaidi. Lakini kupitia mchezo huu vijana wengi wanajipatia ajira tena zenye ujira wenye kuridhisha kabisa na zaidi ni nchi nyingi kufaidika kiuchumi kupita mchezo huu kama vile kwanjia ya michuano mbalimbali inayowaleta pamoja katika eneo moja umati wa watu kutoka maeneo mbalimbali nje na eneo husika.
 Mengi yanafanyika katika harakati za kuufanya mchezo huu kuwa bora kila kukicha, baadhi ya mambo yaliofanyika kupitia mashirikisho ya soka duniani ni pamoja na kuanzisha soka la wanawake na hata kufikia hatua ya kombe la dunia la wanawake na hivyo kutanua wigo, nikimaanisha hapo kabla mchezo huu ulikuwa ukiwahusisha wanaume tu lakini sasa hata wanawake wanajikakamua kwenye pitch. Bila kusahau Shirikisho la mpira wa miguu ulaya(UEFA) kuboresha maamuzi uwanjani kwa kuweka vibendera wanne mmoja kwa kila upande wa pitch. Bila kusahau shirikisho la soka la Uingereza(FA) kuanzisha teknolojia ya goli katika kutambua goli kama ni halali au la.
Jitihada pia zinafanyika katika ngazi za vilabu ikiaminika ya kuwa ubora wa mpira katika timu za taifa unachangiwa zaidi na nguvu kubwa katika vilabu. Katika soka imani ziko nyingi lakini zaidi ninalotaka kuligusia katika kipengele hiki ni wimbi la kuwaamini walioishakuwa wachezaji kuwa mameneja katika timu mbalimbali. Jambo hili linatafsiriwa na wanamichezo kama jambo lenye tija zaidi katika kuleta ladha kamili kisoka kwani meneja aliyeisha kuwa mchezaji ni wazi ya kwamba anatambua ni nini kifanyike uwanjani na nani na katika muda gani na mwisho wa siku kutarajia matokeo mazuri.
Haya yameshuhudiwa na watabe  waliowika enzi hizo na mwisho wa siku kukabidhiwa mikoba ya ukocha.  Baadhi wakiwemo Frank Rijkad aliekuwa akiifundisha Barcelona na hata kufanya makubwa akiwa na masupa staa kama Ronaldinho Gaucho na Samwel Eto’o, Akaja  Pep Gaudiola  aliyekuwa kiungo mkabaji kipindi cha enzi zake na baadae kuwa kocha katika timu ya Barcelona B baadae Barcelona ya wakubwa kuanzia mwaka 2008-2012. Ambapo katika kipindi hicho alifanya maajabu katika tasnia ya soka la vilabu na baadae katika msimu huu kupewa mikoba ya kuinoa klabu mashuhuri duniani  inayosifika kwa  mpira wenye hekima nikimaanisha ina wachezaji wenye sifa za kucheza mpira wenye kasi, nguvu na umakini katika kupiga pasi na kufunga hawa ni Bayern munich mabingwa watetezi wa kombe la UEFA. Wako makocha wengi walio aminiwa na kupewa majukumu hayo na walishafanya makubwa kwenye pitch wakiwemo Meki Mexime ‘’kaptani’’ Seleman Matola, Dunga, Diego Maradona na wengine wengi. Katika wiki hii tumeshuhudia pia klabu ya Ac Milan ikifanya maamuzi mazito kwa kumfukuza aliye kuwa kocha wake Massimiliano Allegri na kumkabidhi mikoba kiungo wa timu hiyo ambaye alikaa kwa kipindi cha miaka kumi mdachi Clarence Seedorf. Yamesemwa mengi na walio wengi na  wengi wao wakitegemea makubwa katika klabu hio iliyokuwa na mwanzo mbaya katika ligi kuu ya Italia maarufu kwa Serie A.
Hizi zooooote ni mbwembwe za soka mchezo unaosadikika kuanza kuchezwa katika nchi ya China (karne ya 2 na 3 Kabla ya Kristu) na kusemekana ya kuwa waingereza ndio walio boresha mchezo huu kama tunavyo uona hivi leo. Soka ndiyo habari ya mjini na vijijini, mashuleni na vyuoni, watoto, vijana, rika la kati na hata wazee Kuongelea soka kila siku.

          waandishi wa makala hii 

Yossima Sitta (mhariri & afisa habari wa goloso)
Yudathadei Kway (msanifu wa habari za kimataifa wa   goloso)

0 comments:

Post a Comment