Pages

Tuesday, 21 January 2014

MAKALA YA INTER BLOCKS CUP MWAZO MASHINDANO HADI HATUA YA MAKUNDI



                           GOLOSO LA SOKA

                  Na Goloso members

                          Inter blocks cup 


MABLOCK YOTE YADHIBITISHA KUSHIRIKA

Waandaaji waliandaa form na kanuni pamoja na sheria za mashidano na kuwapa washiriki wote wa michuano  hii timu zote kumi na mbili(12) yaani Block  E, F, G , F, H , I , J, M, Q, R, S, na T. ila  kwa kuwa hii michuano ilikuwa imelenga kitivo cha elimu timu za block E, F, na J walitoa viingilio kwa sababu wakazi wao wengi si waalimu mfano block(E) wanakaa wanafunzi wa kitivo cha sayansi asilia na mahesabu, block (F) wanakaa kitivo cha afya huku block(J) wakazi wengi wanatoka kitivo cha earth science huku block zingine zikiwa na walimu wengi si hivyo tu bali block (G, H, I, na J) ikiwa na vijana wa kutoka kitivo cha sayansi asilia na mahesabu

HATUA YA MTOANO YAMALIZIKA

Timu kumi na mbili zilipangwa kuanzia hatua ya mtoano kufuzu kwenda hatua ya pili ya makundi waandaaji walichezesha droo kuona nani anapangwa na nani. Wawakilishi wa kila timu kutoka kila block walihudhuria sherehe hiyo ya upangaji wa timu hatua ya mtoano na kupangwa kama ifuatavyo
     Block(E) vs Block (T)
     Block(F) vs Block (P)
     Block (G) vs Block (I)
      Block(J) vs block (S)
     Block (H) vs Block (M)
     Block (Q) vs Block (R)

Timu zilicheza mechi mbili mbili nyumbani na ugenini na timu za block (E, F, H, I, J na R) zilifuzu hatua ya pili ya makundi kwa jumla ya mabao kama ilivyooneshwa hapo chini  kwenye mabano   
     Block(E) vs Block(T)----(5 vs 2)
     Block(F) vs Block(P)---(4 vs 2)
     Block(G) vs Block(I)---(1 vs 2)
     Block(J) vs Block(S)----(2 vs 2) J walifuzu kwa bao la ugenini
     Block(H) vs Block(M)---(4 vs 3)
     Block(Q) vs Block(R)----(1 vs 5)

MAKUNDI  YAPANGA NA MECHI ZIKACHEZWA

Baada ya mechi ya mwisho ya mtoano kati ya block(H) vs block(M) kamati ya mashindano chini ya mrope  na Michael ilipanga makundi mawili A  na B ikiwa kundi A likiwa na timu za block ( E, H na R) Huku kundi B  likiwa na timu za Block (F, I na J) timu zote  zilicheza mechi mbili mbili kwa kila kundi timu za block (H na R) zikifuzu hatua ya nusu fainali kutoka kundi A huku wababe block(I na F ) kutoka kundi la B nao walifuzu hatua ya nusu fainali kama inavyooneshwa hapo chini

                               Group A

                                  P      W      D     L      F       A     GD      Pts
BLOCK(H)                2       2       0      0       5       2         3         6
BLOCK(R)                2       1       0      1       3       4        -1         3      
BLOCK(E)                2       0       0      2       2       4        -2         0     
 
                                  Group B

                                 P       W       D      L      F      A     GD    Pts
BLOCK(I)                2        1        1       0       2      1        1       4
BLOCK(F)               2        0        2       0       2      2        0       2
BLOCK(J)                2        0        1       1       1      2       -1       1

           

           UDHAIFU WA MICHUANO

Waaandaji walishidwa kuweka kanuni ambayo ingeweza kufanya michuano hii kuwa mizuri mfano unakuta refa au kamisaa wanakuwa na timu ambazo wanazisapoti au kuwa kocha wa timu furani kitu ambacho ni hatari katika michuano hii  maana refa anaweza kuchezesha ovyo ili kuikwepesha timu yake isicheze na timu furani hatua inayofuat . Kati ya timu ambazo zimeingia hatua ya nusu fainali block (F,H,I, na R) timu za block R kocha wao ndio refa na kamisaa wa michuano hii, block H muuandaji wa michuano hii ndio kocha mchezaji wa timu yake, block I wanakamati wa michuano hii mmoja ndio kocha wa timu ya block(I) na mfadhiri wa timu yao ndio mjumbe wa kamati ya maandalizi kitu ambacho ni hatari sana katika michuano hii.

 MJINI NA VIJIJINI

Kwa ambao hawajui katika michuano timu zilikuwa na chagamoto timu kutoka kijijni na mjini timu za mjini zilikuwa hatari sana kwa timu ambazo  zimetoka kijijini kati ya timu 12 timu 6 zilikuwa zinatoka kijijini na 6 zilikuwa zinatoka mjini kati ya timu zilizovuka hatua ya mtoano timu 5 kati ya 6 kutoka mjini zilifuzu hatua ya makundi na timu moja kutoka kijijini nayo ilivuka hatua ya makundi hiyo ilikuwa imeonesha ni kwa namna gani timu za mjini zilikuwa vizuri sana kuliko timu za kijijini.


FITINA FITINA

Timu nzima ya goloso  iliweza kuhudhuria mechi zote mwanzo wa michuano mpaka hatua ya mtoano inamalizika kulikuwa na fitina fitina mwanzo wa michuano hadi hatua hii ya nusu fainali waandaji na marefa kulikuwa na timu ambazo  walikuwa wanaziombea zitoke mwazo wa michuano timu hizo ni block(E) (F) na J unajua kwa sababu gan? eti wakazi wa block hizo tajwa hawatoki katika kitivo cha elimu. Ilidhihirika pale mechi ya makundi block(E) vs block(R) ambapo waandaji na wanakamati wote walikuwa wanalisapoti bechi la block (r) kutoa maoni nini kifanyikeee ili waitoe block E ama refa kumpa mawaidha afanye nini kitu ambacho ni hatari tena sana vijana kutoka kariakoo watoto wa madukani block E ama nusura watie mpira kwapani baada ya refa kuonesha mapenzi kwa timu ya block R, mpira ulisimama kwa dak kama 10 timu zikibishana baada ya refa kuamua penati ipingwe kuelekea katika lango la timu ya block(E)



              GOLOSO TUNAMULIKA MBALI

Timu nzima ya goloso ilikuwa inachambua mechi mwanzo wa mechi hadi wa mwisho ilikuwa inaongozwa na mwenyekiti  ATTU GERVAS, katibu wa goloso RAJABU JUMA,  afisa habari na Mhariri wa goloso YOSSIMA SITTA,  wasanifu wa habari za kimataifa wa goloso KWAY YUDATHAEI NA ERICK GWAKISA  na wajumbee NGULLY ALEX, LUKUBA ENDREW, MOLLA JEROME, DANNY JUSTINE, JOSEPH MWAIPUNGU, MASALU, ENOCK  NA  HAMISI



ENDELEA KUFUATILIA WWW.GOLOSOLETU.BLOGSPOT.COM
HATUA YA NUSU FAINALI

0 comments:

Post a Comment